JUMUIYA YA ‘PEPOHUDA’ YATOA MAFUNZO KWA WASICHANA NA MSAADA WA TAULO ZA KIKE.

 Imeandikwa Na, Hassan Msellem.


Mwenyekiti Baraza la Mji Wete Bi. Zulfa Abdalla Saidi, akikabidhi taulo za kike kwa mwanafunzi.

Wanafunzi Kisiwani Pemba wametakiwa kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo mahusiano ya kimapenzi ili kuepukana na madhara yanayoweza kujitokeza.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti Baraza la Mji Wete Bi. Zulfa Abdalla Saidi, wakati akifunga mafunzo ya afya ya uzazi kwa wanafunzi wa Skuli ya Sekondari ya Chasasa yaliyotolewa na Jumuiya kupunguza umaskini na kuboresha maisha ya watu Pemba (PEPOHUDA) huko Jadida Wete, amesema kumekuwepo kwa taarifa za wanafunzi wanaojihusisha na mahusiano ya kimapenzi hali inayopelekea kufanya vibaya katika masomo yao pamoja na kushindwa kuendelea na masomo.


Kwa upande wake mwakilishi kutoka Ofisi ya Mrajis wa jumuiya zisizo za Kiserikali Kisiwani Pemba Bi. Sada Abuubakar Khamis, amesema kutolewa kwa mafunzo hayo afya ya uzazi kwa wanafunzi hao kutawasaidia kukabiliana na changamoto mbali mbali ikiwemo kujikinga na mimba za umri mdogo.


Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mrajis wa jumuiya zisizo za Kiserikali Kisiwani Pemba Bi. Sada Abuubakar Khamis.

Mratibu wa Jumuiya ya Pepohuda Said Mbarouk Juma, alisema utolewaji wa mafunzo hayo ni mwendelezo wa utekelezaji wa mradi wa kuongeza uelewa wa haki za afya ua uzazi kwa watoto na vijana wa kike ili kuwakinga na mimba za umri mdogo.

Mratibu wa Jumuiya ya PEPOHUDA Said Mbarouk Juma.

Akiwasilisha mada ya Mawasiliano na Madhara ya Mimba za umri mdogo Bi. Hudhaifa Said Salum, amesema miongoni mwa madhara yanayoweza kujitokeza katika mimba za umri mdogo ni pamoja na kukatisha masomo, kupoteza damu nyingi kipindi cha kujifungua pamoja vifo.

Muwasilishaji mada kutoka taasisi ya Umati Hudhaifa Said Salum.

Katika kukabilaiana na vitendo vya udhalilishaji Mkufunzi wa mafunzo hayo Mwanaisha Amani Salum, aliwataka wasichana hao kutoa taarifa pindi wanapofanyiwa vitendo hivyo pamoja na kujiepusha na marafiki waovu.


Sheha wa Shehia ya Mtemani Mrisho Juma Mtumwa, aliwasihi wanafunzi hao kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili yaweze kuwasaidia masomo yao.


Nao wanafunzi hao wameishukuru jumuiya ya PEPOHUDA kwa kuwapatia mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi ili lengo la utolewaji wa mafunzi hayo liweze kufikiwa.

Wanafunzi wa Skuli ya Chasasa Wete wakichangia mada.

Mafunzo hayo ya siku moja yametoelewa na jumuiya kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu Pemba ‘PEPOHUDA’ kwa ufadhili wa Shirika la Y+ Global kupitia mfuko wa Her Voice Fund.


Comments

Popular posts from this blog

"Kumalizika kwa mradi wa SWIL isiwe sababu ya kubweteka kuzifanyia kazi changamoto za kijamii-CB" DC Chake Chake.