TAMWA, PEGAO NA ZAFELA ZAFANYA ZIARA VIJIJINI KUANGALIA MAFANIKIO NA CHANGAMOTO ZA WANANCHI-MRADI WA SWIL.
IMEANDIKWA NA HASSAN MSELLEM, PEMBA. Katika kutamatisha uketelezaji wa mradi wa Uhamasishaji wa Wanawake katika Uongozi (SWIL) chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania ‘TAMWA’ Jumuiya Utetezi wa Mazingira na Kijinsia Pemba ‘PEGAO’ na Chama cha Wanasheria Wanawake Zanzibar ‘ZAFELA’ zimefanya ziara maalumu ya kuangalia mafanikio na kusikiliza changamoto katika Skuli ya Msingi Kunguni na Familia yenye watoto watano wenye ulemavu wa viungo katika kijiji cha Kwa-Azani Wambaa ili kuweza kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo. Rashid Omar Ali, ni mwalimu Mkuu wa Skuli ya Msingi Kunguni amesema kupitia mradi wa SWIL wamefanikiwa kuongeza idadi ya vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo pamoja na walimu, mafanikio ambayo yamechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya ufaulu kwa wanafunzi wa darasa la saba kutoka wanafunzi wawili mwaka 2022 hadi wanafunzi saba mwaka 2023. Aidha amesema licha mafanikio hayo bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji na kuz...